• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Manispaa ya Kahama
Halmashauri ya Manispaa ya Kahama

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Kahama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango, Uchumi na Takwimu
      • Maendeleo Ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Ukaguzi
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Habari
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Usafi na Mazingira
    • Maendeleo ya Jamii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Kamati ya Fedha na Utawala
      • Kamati ya Mipango Miji na Mazingira
      • Kamati ya Uchumi, Elimu na Afya
  • Miradi
    • Miradi iliyopitishwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria
      • Sheria ndogo za mazingira
      • Sheria ndogo za Halmashauri
      • Tozo za Leseni za Biashara
    • Fomu
    • Miongozo
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio
    • Habari

Wadau wa Elimu Kahama wakutana kujadili Maendeleo ya Elimu, Maazimio ya kufanikisha yafikiwa.

Imewekwa: December 20th, 2017

Uhitaji wa vyumba vya madarasa ni changamoto kubwa katika sekta ya elimu hivi sasa. Kwa kulitambua hilo wadau wa Elimu Mji wa Kahama wamekutana leo kujadili namna gani changamoto hiyo inaweza kutatuliwa. Baada ya mjadala mrefu wadau hao kila mmoja kwa nafasi yake alitoa ahadi ya mchango na pia maazimio 6 yameafikiwa kwa pamoja ambayo ni:

  • Kila Kaya ichangie  kuanzia Shilingi 10,000 na kuendelea.
  • Vifanyike Vikao vya kushirikisha Wadau  kwa makundi  yao mapema Mfano:Wafanyabiashara, Taasisi za Elimu, Waendesha  Pikipiki.
  • Mkurugenzi na Timu yake watembelee Wadau / Mdau mmoja mmoja.
  • Mkurugenzi  na Timu yake watembelee  vyombo vya habari vyote vilivyopo Kahama ili kutengeneza jingo ya kuhamasisha uchangiaji Elimu kwa wadau wa ndani na nje ya Kahama.
  • Kuaandaa Tamasha maaluum kwa ajili ya uchangiaji Sekta ya Elimu.
  • Uchangiaji uwe ni Fedha Taslimu au Vifaa vya Ujenz kadri Mdau anavyoguswa.
  • Kila Mkuu wa Idara aunde Kamati ya uhamasishaji ya Kata ambayo haitahusisha wanasiasa, Kamati hiyo ihusishe wafanyabiashara, Watu maarufu, Viongozi wa Dini na Watendaji wa Kata.
  • Vikao vya Wadau vipangiwe ratiba.
  • Ifanyike tathmini ya shughuli 

Katika taarifa iliyoandaliwa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Kahama kwa Wadau hao inaonesha kuwa Halmashauri ya Mji wa Kahama Mwaka 2017 ilikuwa na jumla ya wanafunzi 69,043 kwa madarasa ya awali hadi la saba. Kulikuwa na mahitaji ya vyumba vya madarasa 1,534, vilikuwepo 618 na upungufu   916. Idadi ya wanafunzi waliohitimu darasa la saba 2017  ni 5,391 na wanaotarajiwa kuandikishwa darasa la awali na la kwanza ni wanafunzi 25,303, Hii ni sawa na ongezeko la  la wanafunzi 19,912, hivyo kufanya upungufu wa vyumba vya madarasa  1,359,Madawati 9,128 na Matundu ya vyoo  796

Pia kwa upande wa Elimu Sekondari Mwaka 2017 ilikuwa na jumla ya wanafunzi 8,721 kuanzia  Kidato cha Kwanza hadi Kidato cha Sita,  Kulikuwa na mahitaji ya vyumba vya madarasa  214, vilikuwepo 161 na upungufu   53. Idadi ya wanafunzi waliohitimu kidato cha Nne Mwaka 2017  ni 1,456 na wanaotarajiwa kusajiliwa Kidato cha Kwanza 2018 ni Wanafunzi 4,184, Hii ni sawa na ongezeko la  la Wanafunzi 2,728 , hivyo kufanya upungufu wa vyumba vya Madarasa  102 ,Viti na meza 2,659 na matundu ya vyoo 348.

GHARAMA ZINAZOHITAJIKA KUONDOA MAPUNGUFU HAYA.

S/N
IDARA
MIUNDOMBINU HITAJIKA
IDADI
GHARAMA@
JUMLA
01
ELIMU MSINGI
MADARASA
1359
6,169,687.5
8,384,605,312.5
MADAWATI
9,128
70,000
638,960,000
VYOO
796
1,000,000
796,000,000
JUMLA
 
 
9,819,565,312.5
02
ELIMU SEKONDARI
MADARASA
102
6,169,687.5
629,308,125
VITI NA MEZA
2,659
70,000
186,130,000
VYOO
348
1,000,000
348,000,000
JUMLA
 
 
1,163,438,125
 

JUMLA YA GHARAMA YOTE

10,983,003,438

 

Gharama za madarasa ni za ukamilishi baada ya nguvu za wananchi kujenga boma.

MIKAKATI YA HALMASHAURI

UWEZO WA HALMASHAURI

Halmashauri imetenga kiasi cha Tshs 725,073,031.60  kwenye bajeti yake ya mwaka wa Fedha 2017/2018. Na fedha hiyo itakusanywa katika vyanzo mbalimbali vya mapato ya ndani hadi mwezi Juni 2018.

MCHANGO WA JAMII

Halmashauri imehamasisha jamii kupitia vikao vya Mendeleo ya Kata  kushiriki katika kuchangia ujenzi wa maboma ya vyumba vya madarasa, zoezi ambalo linaendelea mpaka sasa.

KUSHIRIKISHA WADAU MBALIMBALI WA MAENDELEO.

Halmashauri imepanga kukutana na wadau mbalimbali wa maendeleo kwa ajili ya kujadili kwa pamoja utatuzi wa mapungufu haya ili ifikapo tarehe 08/01/2018 wanafunzi wapate mahali pa kujifunzia.


Matangazo

  • INGIA HAPA KUPATA SALARY SLIP YAKO June 03, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI

    May 14, 2025
  • Kanuni za Maadili za Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2025

    April 19, 2025
  • Uboreshaji Awamu ya Pili wa Daftari la Mpiga Kura kuanza Mei Mosi

    April 16, 2025
  • Naibu Meya Manispaa ya Kahama ahimiza Ulipaji wa Ankara za Hati

    April 16, 2025
  • Angalia zote

Video

Ufafanuzi wa Mikopo ya Asilimia Kumi Manispaa ya Kahama
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Picha Mbalimbali
  • Matukio Mbalimbali
  • Kupata Salary slip
  • Mapato na Matumizi Oktoba -Desemba 2017
  • Taarifa ya Miradi ya Mwaka 2016/2017
  • Zabuni mbalimbali
  • Taarifa kwa umma

Viunganishi vinavyohusiana

  • MFUMO WA KUWASILISHA MALALAMIKO
  • Ajira Serikalini
  • NECTA
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Tovuti ya Ikulu

Wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    Barabara ya Boma, Kahama

    Anuani ya Posta: P.O.Box 472

    Simu: +255 282710032

    Simu: +255719679464

    Barua pepe: md@kahamamc.go.tz / info@kahamamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2017. Halmashauri ya Manispaa Kahama. Haki zote zimehifadhiwa