• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Manispaa ya Kahama
Halmashauri ya Manispaa ya Kahama

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Kahama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango, Uchumi na Takwimu
      • Maendeleo Ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Ukaguzi
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Habari
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Usafi na Mazingira
    • Maendeleo ya Jamii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Kamati ya Fedha na Utawala
      • Kamati ya Mipango Miji na Mazingira
      • Kamati ya Uchumi, Elimu na Afya
  • Miradi
    • Miradi iliyopitishwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria
      • Sheria ndogo za mazingira
      • Sheria ndogo za Halmashauri
      • Tozo za Leseni za Biashara
    • Fomu
    • Miongozo
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio
    • Habari

Serikali yaingilia Kati Suala la Bei ya Pamba

Imewekwa: July 17th, 2019

Waziri wa Kilimo Mhe. Japhet Hasunga amesema kuwa bei ya Pamba itabaki kuwa Shilingi 1,200 hata kama imeshuka kwenye Soko la dunia. Amesema hayo mapema leo alipokuwa akiongea na Wakulima wa Pamba Wilayani Kahama kwenye vituo vya kuuzia Pamba.

"Wadau walikutana wakapanga bei na iliafikiwa kuwa mwaka huu bei ni 1200 kwa kilo ya Pamba.
Lakini baada ya msimu kuanza soko la dunia likashuka. Baada ya kukokotoa ikaonekana inabidi Pamba iuzwe kwa shilingi 900 kwa kilo, hali hii ikawashtua wanunuzi wakaona bei haina faida tena kwa upande wao. Lkn Serikali ikasema hapana lazima wanunuzi wanunue kwa 1200 na hiyo hasara itafidiwa na Serikali. Serikali itawalipa wanunuzi 300 ili Mnunuzi aendelee kumlipa mkulima shilingi 1200 badala ya 900". Amesema Mhe. Hasunga
Aidha Mhe. Hasunga amesema kuwa Serikali imeshafanya mkakati wa kushirikisha Benki kuu ili Mabenki yawashushie riba wafanyabiashara wenye nia ya kununua pamba. Na ameagiza kuwa ifikapo tarehe 31 Julai mwaka huu pamba yote iwe imenunuliwa na wakulima wote wawe wamelipwa hela zao.

Katika hatua nyingine Mhe. Hasunga ameagiza kuwa kuanzia mwakani hakuna mkulima atakayekopeshwa pembejeo hivyo wakulima wakiuza Pamba yao watenge hela ya kununulia pembejeo ikiwemo dawa na mbolea. Amesema hii itasaidia kuwafanya wakulima wanunue dawa wanazoziamini wao badala ya kulazimishwa dawa ambazo nyingi zinakuwa hazina ufanisi.

Mhe. Hasunga yupo kwenye ziara ya kikazi Wilayani hapa kwa siku moja na ametembelea vituo vya kuuzia Pamba na kuongea na wakulima kila kituo.

Matangazo

  • INGIA HAPA KUPATA SALARY SLIP YAKO June 03, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI

    May 14, 2025
  • Kanuni za Maadili za Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2025

    April 19, 2025
  • Uboreshaji Awamu ya Pili wa Daftari la Mpiga Kura kuanza Mei Mosi

    April 16, 2025
  • Naibu Meya Manispaa ya Kahama ahimiza Ulipaji wa Ankara za Hati

    April 16, 2025
  • Angalia zote

Video

Ufafanuzi wa Mikopo ya Asilimia Kumi Manispaa ya Kahama
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Picha Mbalimbali
  • Matukio Mbalimbali
  • Kupata Salary slip
  • Mapato na Matumizi Oktoba -Desemba 2017
  • Taarifa ya Miradi ya Mwaka 2016/2017
  • Zabuni mbalimbali
  • Taarifa kwa umma

Viunganishi vinavyohusiana

  • MFUMO WA KUWASILISHA MALALAMIKO
  • Ajira Serikalini
  • NECTA
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Tovuti ya Ikulu

Wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    Barabara ya Boma, Kahama

    Anuani ya Posta: P.O.Box 472

    Simu: +255 282710032

    Simu: +255719679464

    Barua pepe: md@kahamamc.go.tz / info@kahamamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2017. Halmashauri ya Manispaa Kahama. Haki zote zimehifadhiwa