• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Manispaa ya Kahama
Halmashauri ya Manispaa ya Kahama

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Kahama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango, Uchumi na Takwimu
      • Maendeleo Ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Ukaguzi
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Habari
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Usafi na Mazingira
    • Maendeleo ya Jamii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Kamati ya Fedha na Utawala
      • Kamati ya Mipango Miji na Mazingira
      • Kamati ya Uchumi, Elimu na Afya
  • Miradi
    • Miradi iliyopitishwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria
      • Sheria ndogo za mazingira
      • Sheria ndogo za Halmashauri
      • Tozo za Leseni za Biashara
    • Fomu
    • Miongozo
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio
    • Habari

Rais azindua kiwanda cha Kuchakata vyuma Wilayani Kahama

Imewekwa: March 11th, 2018

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli asubuhi ya leo amezindua kiwanda cha kuchakata vyuma eneo la Nyasubi Wilayani Kahama. Akiwa kwenye uzinduzi huo Rais ameahidi kusimamia sekta ya viwanda kwa hali na mali na amewaomba mawaziri na viongozi wa ngazi mbalimbali kuendelea kuvithamini viwanda vya ndani na kutumia bidhaa zinazotengenezwa ndani ya nchi. 

"Niwatake wakandarasi na viongozi wa Wizara, hususan Wizara ya Maji, na ninaposema wizara ya maji namaanisha taasisi zote zinazoshughulika na Maji zikiwemo Halmashauri wanapokuwa na Miradi ya Maji ni vyema wakatumia mabomba yaliyotengenezwa na wazawa, wakikosa ndio wafikirie kutafuta nje" Amesema Rais

Aidha Mhe. Rais amewaasa wamiliki wa viwanda wazawa kutengeneza bidhaa zenye ubora ili waweze kuaminika. Amesema kuwa kutengeneza bidhaa zilizo chini ya kiwango ndio sababu ya watu kuzikimbia bidhaa za ndani.

Awali akisoma taarifa ya Kiwanda hiko, Mkurugenzi wa Kahama Oil Mill & Companies Bw. Mhoja amebainisha changamoto kadhaa zinazoathiri uendeshaji mzuri wa Kiwanda hiko. Kuwepo kwa Kodi kubwa katika uingizaji wa bidhaa za viwanda ni changamoto mojawapo inayosababisha kushuka kwa uzalishaji. 

Akilijibu suala kodi Mhe. Rais ameshauri mmiliki wa kiwanda kufikiria kuanzisha kiwanda cha uchimbaji chuma badala ya kuagiza chuma kilichokamilika kutoka nje ambacho katika misingi ya kodi inachajiwa kama bidhaa iliyokamilika badala ya Malighafi.

"wewe niambie unataka eneo lenye ukubwa gani ili uanzishe uchimbaji wa chuma, sheria za kodi zitaendelea kubana iwapo utaendelea kuagiza vyuma kutoka nje, mimi nitakupa hilo eneo bure" amesema Rais.

Mhe. Rais ameshahitimisha ziara yake Mjini Kahama na ameshaondoka kuelekea Singida na Dodoma.

Matangazo

  • INGIA HAPA KUPATA SALARY SLIP YAKO June 03, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI

    May 14, 2025
  • Kanuni za Maadili za Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2025

    April 19, 2025
  • Uboreshaji Awamu ya Pili wa Daftari la Mpiga Kura kuanza Mei Mosi

    April 16, 2025
  • Naibu Meya Manispaa ya Kahama ahimiza Ulipaji wa Ankara za Hati

    April 16, 2025
  • Angalia zote

Video

Ufafanuzi wa Mikopo ya Asilimia Kumi Manispaa ya Kahama
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Picha Mbalimbali
  • Matukio Mbalimbali
  • Kupata Salary slip
  • Mapato na Matumizi Oktoba -Desemba 2017
  • Taarifa ya Miradi ya Mwaka 2016/2017
  • Zabuni mbalimbali
  • Taarifa kwa umma

Viunganishi vinavyohusiana

  • MFUMO WA KUWASILISHA MALALAMIKO
  • Ajira Serikalini
  • NECTA
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Tovuti ya Ikulu

Wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    Barabara ya Boma, Kahama

    Anuani ya Posta: P.O.Box 472

    Simu: +255 282710032

    Simu: +255719679464

    Barua pepe: md@kahamamc.go.tz / info@kahamamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2017. Halmashauri ya Manispaa Kahama. Haki zote zimehifadhiwa