• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Manispaa ya Kahama
Halmashauri ya Manispaa ya Kahama

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Kahama

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango, Uchumi na Takwimu
      • Maendeleo Ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Ukaguzi
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Habari
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Usafi na Mazingira
    • Maendeleo ya Jamii
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Kamati ya Fedha na Utawala
      • Kamati ya Mipango Miji na Mazingira
      • Kamati ya Uchumi, Elimu na Afya
  • Miradi
    • Miradi iliyopitishwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria
      • Sheria ndogo za mazingira
      • Sheria ndogo za Halmashauri
      • Tozo za Leseni za Biashara
    • Fomu
    • Miongozo
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio
    • Habari

Barrick Buzwagi yakabidhi hundi ya Kodi ya huduma kwa Mji wa Kahama

Imewekwa: July 15th, 2020

Kampuni ya uchimbaji madini ya Twiga Minerals Corporation kupitia mgodi wake wa dhahabu wa Barrick Buzwagi imekabidhi hundi yenye thamani ya shilingi Bilioni 1.15 (1,159,817,107.83/=) kwa halmashauri ya Mji wa Kahama  ikiwa ni malipo ya ushuru wa huduma kwa kipindi cha kuanzia mwezi Januari hadi Juni 2020.

Akikabidhi hundi hiyo kwa Mkuu wa wilaya ya Kahama, Mhe. Anamringi Macha leo Jumatano Julai 15,2020,Meneja Mkuu wa Mgodi wa Buzwagi, Benedict Busunzu amesema lengo la mgodi huo ni kuona mamlaka husika zinaelekeza fedha hizo katika miradi inayolenga kuwaletea maendeleo wananchi wanaozunguka migodi.

“Migodi ya Twiga Minerals chini ya Kampuni ya Barrick nchini Tanzania hulipa ushuru wa huduma kila baada ya miezi sita kwa halmashauri ili ambazo migodi yetu inaendesha shughuli zake kulingana na mapato ya kila mwaka ambapo malipo haya ni kutekeleza hitaji la kisheria na ni sehemu ya mikataba ya makubaliano kati ya migodi na halmashauri husika”,aliongeza Busunzu.

“Tunatoa ushuru ili kuboresha utoaji wa huduma katika jamii zinazozunguka migodi katika sekta mbalimbali ikiwa ni pamoja na elimu,afya na upatikanaji wa maji safi na salama”,alisema.

Aidha alisema licha ya mgodi huo kulipa kodi stahiki bado imekuwa ikijishughulisha katika kuhakikisha inakuwa mdau muhimu wa maendeleo kupitia sera yake ya maendeleo ya jamii  ikiwa ni kuunda fursa endelevu za kiuchumi na maendeleo  katika jamii na kuinua uchumi wa wilaya na kuboresha ustawi wa maisha ya wenyeji.

Akipokea hundi hiyo, Mkuu wa wilaya ya Kahama,Mhe. Anamringi Macha aliipongeza kampuni ya Twiga Minerals kwa kutoa ushuru wa huduma ikiwa ni zao la kwanza chini ya Twiga iliyotokana na ubia kati ya serikali na Barrick huku akiiagiza halmashauri kutumia fedha hizo kwa utaratibu utakaoleta tija kwa wananchi.
“Sisi tunataka fedha zinaenda kwenye miradi ambayo itakuwa na tija kwa ajili ya maendeleo ya vijana, watu wenye ulemavu,wanawake. Mkono wa serikali bado upo pale pale kuhakikisha fedha hizi zinakwenda kutekeleza ile miradi tuliyoikusudia”,alisema Macha.

Alisema fedha hizo zitatumika kutekeleza miradi ya maendeleo katika jamii ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika sekta ya elimu,afya,maji na miradi mingine itakayogusa wananchi moja kwa moja.


Matangazo

  • INGIA HAPA KUPATA SALARY SLIP YAKO June 03, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI

    May 14, 2025
  • Kanuni za Maadili za Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani 2025

    April 19, 2025
  • Uboreshaji Awamu ya Pili wa Daftari la Mpiga Kura kuanza Mei Mosi

    April 16, 2025
  • Naibu Meya Manispaa ya Kahama ahimiza Ulipaji wa Ankara za Hati

    April 16, 2025
  • Angalia zote

Video

Ufafanuzi wa Mikopo ya Asilimia Kumi Manispaa ya Kahama
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Picha Mbalimbali
  • Matukio Mbalimbali
  • Kupata Salary slip
  • Mapato na Matumizi Oktoba -Desemba 2017
  • Taarifa ya Miradi ya Mwaka 2016/2017
  • Zabuni mbalimbali
  • Taarifa kwa umma

Viunganishi vinavyohusiana

  • MFUMO WA KUWASILISHA MALALAMIKO
  • Ajira Serikalini
  • NECTA
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Tovuti ya Ikulu

Wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    Barabara ya Boma, Kahama

    Anuani ya Posta: P.O.Box 472

    Simu: +255 282710032

    Simu: +255719679464

    Barua pepe: md@kahamamc.go.tz / info@kahamamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2017. Halmashauri ya Manispaa Kahama. Haki zote zimehifadhiwa